Monday, April 25, 2016

PAPA WEMBA MUIMBAJI WA CONGO ALIANGUKA AKIWA JUKWAANI NA KUFARIKI DUNIA

Muimbaji Maarufu toka Congo Papa Wemba afariki Dunia akiwa na Miaka 66 aki anguka jukwaani akiwa anaimba, 



Video zinaonyesha akianguka jukwaani nyuma ya wachezaji mziki wake kabla ya kupata huduma ya kwanza

Mwana Muziki huyo alijijengea umaarufu mkubwa kwa miondoko yake yaki Afrika  huku aki changanya na miondoko yaki Cuban na kufanya mziki wake kuwa mziki waki pekee na maarufu sana duniani.

Mwana Mziki huyu aliwahi kuzunguka nchi nyingi sana duniani akifanya matamasha mbalimbali, aliwahi pia kufanya nyimbo na mwanamziki maarufu wa wingereza  Peter Gabriel. Papa wemba kafanya mengi katika mziki wa Congio na Africa kwa ujumla wqwatu wengi wamejalibu kumfananisha na msanii Fela Kuti kwa ustadi wa mziki Africa. 

Papa Wemba alianza kujiskia ni mgonjwa siku ya Jumamosi asubuhi na baadaye kuiaga dunia akiwa jukwaani ila sababu za kifo chake mpaka sasa hazijulikani

Alifariki wakiwa bado hawajamfikisha Hospitalini kwa taarifa zilizo tolewa na msemaji wa police wa Ivosep Morgue huko Abjdan 

Mwanamziki huyu alizaliwa mwaka 1949 majina yake ya kuzaliwa yakiwa ni Shungu Wembadio Pene Kikumba aliaza kugundua kipaji chake cha kuimba ikiwa kama muimba kwaya wa kanisani.

Papa Wemba ni msanii aliye saidia sana kukuza mziki wa Congo wa miondoko ya Rhumba kwa style zake za Soukous ambazo zimekuja kuwa ni maarufu sana nchini Africa. 

Pamoja na band yake ya mziki ya Zaiko Langa Langa, Isifi na Viva la Musica wameweza kufanya hits nyingi ikiwemo L'Escrave na le Voyageur.




No comments:

Post a Comment