Thursday, June 15, 2017

MWANAMZIKI KING KAKA WA KENYA APEWA KAZI NA UMOJA WA MATAIFA




Mwanamuziki maarufu King Kaka amechaguliwa kuwa balozi wa shirika la umoja wa mataifa la huduma kwa watoto,UNICEF -Kaka alitangaza habari hiyo njema kwenye mtandao wake wa kijamii wa Instagram Mwanamuziki maarufu wa nyimbo za aina ya Rap,Kaka King Ametupia ujumbe kwenye mtandao wake wa instagram

siku ya jumatano.mwanamuziki huyo alizindua nyimbo mpya inayoitwa ’Yap Yap’. Bila kuchelewa siku iliyofuata King aka dondosha  ngoma nyingine mpya na kupa jina  ‘Life na adabu’. Kando na hayo mwanamuziki huyo amechaguliwa kuwa balozi wa shirika la umoja wa mataifa la huduma kwa watoto, UNICEF. Akionyesha furaha yake kwenye ujumbe aliouchapicha kwenye ukurasa wake wa Instagram, King alisema kufanikiwa kwake kunatokana na bidii.
 “ Ungana nami ninaposhirikiana na shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto, UNICEF kujadili jinsi ya kuishi maisha bila tashwishwi,”King aliandika kwenye ukurasa wake wa Instagram. King anajulikana kwa miziki zake zilizovuma kama,Niko kwa jam nakam Dodoma. Swahili shakespere nazingine nyingi.

No comments:

Post a Comment